Atakayeshuka mahali akasema: Audhubikalimaatillaahit-taammaati min sharri maa khalaqa (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyotimia kutokana na shari ya vile alivyoviumba) hakitomdhuru kitu mpaka aondoke mahala pake hapo

Atakayeshuka mahali akasema: Audhubikalimaatillaahit-taammaati min sharri maa khalaqa (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyotimia kutokana na shari ya vile alivyoviumba) hakitomdhuru kitu mpaka aondoke mahala pake hapo

Kutoka kwa Khaula bint Hakim As-Sulamiyya, amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema: "Atakayeshuka mahali akasema: Audhubikalimaatillaahit-taammaati min sharri maa khalaqa (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyotimia kutokana na shari ya vile alivyoviumba) hakitomdhuru kitu mpaka aondoke mahala pake hapo".

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]

الشرح

Anauelekeza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- umma wake katika kushikamana na kukimbilia kwenye tija ambako hutoeka kila chenye kuogofya anachokiogopa mwanadamu pale anaposhuka mahali katika ardhi, sawa sawa awe safarini au matembezini na kwingineko: Kuwa ajikabidhi na atake ulinzi kupitia maneno ya Allah yaliyotimia katika fadhila zake na baraka zake na manufaa yake, yaliyosalimika na kila aibu na mapungufu, kutokana na shari ya kila kiumbe chenye shari, ili awe na amani katika mazingira yake hayo kwa muda wote atakaokuwa hapo kutokana na kila chenye kuudhi.

فوائد الحديث

Kutaka ulinzi ni ibada, nako ni kule kunakokuwa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu au kwa majina yake na sifa zake.

kufaa kutaka ulinzi kupitia majina ya Mwenyezi Mungu, kwa sababu majina hayo ni sifa miongoni mwa sifa za Mwenyezi Mungu Mtukufu, kinyume na kutaka ulinzi kwa kiumbe yeyote kwani hii ni shirki.

Ubora wa dua hii ni baraka zake.

Kujikinga kupitia adhkari ni sababu ya mja kulindwa na shari.

Kubatilika kutaka ulinzi kutoka kwa asiyekuwa Allah miongoni mwa Majini na wachawi na matapeli na wengineo.

Sheria ya dua hii kusomwa na mwenye kushuka mahali nyumbani au safarini.

التصنيفات

Adhkaar za mambo ya Dharura.