Atakayeisahau swala, basi aiswali atakapoikumbuka, haina kafara nyingine isipokuwa hiyo

Atakayeisahau swala, basi aiswali atakapoikumbuka, haina kafara nyingine isipokuwa hiyo

Kutoka kwa Anasi bin Maliki -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Atakayeisahau swala, basi aiswali atakapoikumbuka, haina kafara nyingine isipokuwa hiyo: "Na simamisha swala kwa ajili ya kunitaja mimi" [Twaha: 14].

[Sahihi] [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

الشرح

Amebainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa atakayesahau kutekeleza swala ya faradhi mpaka ukatoka wakati wakati wake, basi anatakiwa aende mbio na afanye haraka kuilipa pale anapoikumbuka, amesema Allah katika kitabu chake kitukufu: "Na usimamishe swala kwa ajili ya kunitaja" [Twaha: 14] Simamisha swala zilizosahaulika unapozikumbuka.

فوائد الحديث

Umuhimu swala na kutozembea katika kuitekeleza na kuilipa.

Haitakiwi kuichelewesha swala nje ya wakati wake kwa makusudi bila udhuru.

Uwajibu wa kulipa swala kwa aliyesahau na aliyesinzia mpaka atakapo amka.

Uwajibu wa kulipa swala haraka hata kama ni katika nyakati zilizoharamishwa.

التصنيفات

Wajibu wa Swala na Hukumu ya Mwenye kuiwacha., Makosa ya wenye kusali.