Je, wasikia wito wa swala?" Akasema: Naam, akasema: "Basi ujibu

Je, wasikia wito wa swala?" Akasema: Naam, akasema: "Basi ujibu

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Mtu mmoja kipofu alimjia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika mimi sina muongozaji wa kunileta msikitini, akamuomba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amruhusu asali nyumbani kwake, akamruhusu, alipoondoka akamuita, akasema: "Je, wasikia wito wa swala?" Akasema: Naam, akasema: "Basi ujibu".

[Sahihi] [Imepokelewa na Imamu Muslim]

الشرح

Mtu mmoja kipofu alimjia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika mimi sina wa kunisaidia na kunishika mkono kuja msikitini, katika swala tano, akitaka Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amruhusu, alipompa mgongo alimuita na akasema: Je, unasikia adhana ya swala? akasema: Ndiyo, akasema: Basi mjibu anayenadi kwa ajili ya swala.

فوائد الحديث

Uwajibu wa swala ya jamaa; kwa sababu kutaka ruhusa huwa hakuwi ila kwa jambo la lazima.

Kauli yake: "Mjibu" Kwa mwenye kusikia wito inaonyesha kuwa swala ya pamoja ni lazima; kwa sababu asili ya amri ni wajibu.

التصنيفات

Ubora wa Swala ya Jamaa na Hukumu zake.