إعدادات العرض
1- Tulimuunga mkono Mtume rehema na Amani zimfikie- juu ya usikivu na Utii katika ugumu na wepesi, na katika raha na karaha, na hata kwa kujinyima sisi, nakuwa tusizozane na watu katika jambo wanalostahiki.
2- Hakika watakuongozeni nyinyi viongozi ambao watafanya mambo mtayajua na mengine hamtoyajua, atakayechukia atakuwa kajiepusha, na atakayepinga atakuwa kasalimika, lakini atakaye ridhia na akafuatisha, wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kwanini tusiwapige vita? Akasema: Hapana, madam bado wanasimamisha kwenu nyinyi swala
3- Atakayejitoa katika utiifu< na akasambaratisha umoja akafa atakuwa kafa kifo cha zama za kijinga,na atakayepigana chini ya bendera ya kibubusa nachukia kwa kuwapendelea ndugu zake,au akahamasisha (kupendelea kwa sababu) ya ndugu zake au anaunusuru udugu akauwawa,basi hicho ni kifo cha zama za ujinga
4- Yeyote atakaye kujieni na akakuamrisheni nyote muwe dhidi ya mtu mmoja, akataka kupasua nguvu yenu, na usambaratishe umoja wenu, basi muuweni